Jumanne, 18 Agosti 2015

CCM YATANGAZA KAMATI YA KUMWANGAMIZA LOWASA.

Dar es salaam    
                                                                      Agost 18.2015

Ikiwa zimebaki siku tatu filimbi ya kuanza kampeni za Uchaguzi Mkuu kuanza ambapo ni Agost 22 mwaka huu,Chama cha Mapinduzi kimetangaza rasmi wajumbe wa kamati ya kampeni ya kitaifa yya chama hicho.

Akitangaza kamati hiyo leo katibu wa halmashauri kuu ya TAIFA,Itikadi na Uenezi Nape Mnauye amesema kuwa kamati hiyo itakua na wajumbe 32 ambao wataongozwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Abdulrahman Kinana, makamu mwenyekiti bara Rajabu Luhwavi na makamu mwenyekiti Zanzibar Vuai Ali Vuai.

Wajumbe wengine ni Sofia Simba,Mohamed Seif Khatib,Asha Rose Migiro,Samweli Sitta,Nape Mnauye,Mwigulu Nchemba,Harrisoni Mwakyembe,January Makamba,Amina Makillagi,Christpher Ole Sendeka,Stephen Wasira, Abdallah Bullembo,Hadija Aboud,Mohamed Aboud,Lazaro Nyalandu,Issa Haji Ussi,Waride Bakari Jabu.

Wengine ni Mohamoud Thabit Kombo,Shamsi Vuai Nahodha,Maua Daftari,Stephen Masele,Pindi Chana,Shaka Shaka,Makongoro Nyerere,Benard Membe,Sadifa Juma Khamisi,Anthony Diallo,Livingston Lusinde pamoja na Ummy Mwalimu.
KUVULIWA WADHIFA NDANI YA CHAMA.

Hivi karibuni kuna taarifa zimekuwa zikisambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Nape Mnauye anavuliwa wadhifa wake huo kwa kile kinachodaiwa anaenda kinyume na maadili ya kazi hiyo,hata hivyo amekanusha nakusema kuwa nitaarifa zisizo na ukweli ndani yake .

“Sijajua hata mimi kwanini taarifa hizi zinasambazwa kwenye mitandao ya kijamii,lakini siyo mimi peke yangu ambaye nimesambaziwa taarifa za nammna hii,nadhani ni dalili mbaya za ukawa ,injini yao inatoa moshi sana na hii ni kutokana na kuchukua oili chafu(Lowasa) ”.alisema Mnauye.
USHINDI NDANI YA CCM.

Kuhusu ushindi wa Uchaguzi Mnauye amesema kuwa CCM itashinda kwa kishindo kutokana na Mgombea wa Urais kupitia vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi Ukawa ambaye pia ni waziri wa mstaafu Edward Lowasa kuwa na kashfa za ubadhilifu wa fedha ikiwemo Richmond.
“Ukijua tekniki za vita na anayeongoza ni komredi kinana ni mtaalamu wa stretejia za vita subirini mapigo yake,nando maana taunasema tutampiga asubuhi tu,na nafikiri siku hiyo ya uchaguzi nivizuri ambulance mbili zisogezwe kwake kwasababu baala atakayoipa hatasahau maishani mwake,huwezi kuchukua fisadi mwizi na aliyekataliwa na Mwalimu Nyerere.”alisema.

Kuhusu ratiba ya uzinduzi wa kampeni ya CCM katibu huyo mwenerzi amesema ratiba itatangazwa muda wowote baada ya mambo kukamilika .
Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa imefanya kikao chake cha siku moja Agost 17 katika Ofisi zake Ndogo za zilizopo mtaa wa Lumumba jijini Dar es salaam Chini ya Mwenyekiti wake Rais Dokta Jakaya Kikwete na kuteuwa wagombea ubunge majimbo mawili ya Singida Mashariki na Kiteto.

Walioteuliwa kupeperusha bendera kwenye majimbo hayo ni Jonathan Njau(Singida Mashariki) na Emmanueli Papian Jonh(Kiteto) ambapo pia hapo jana majimbo yapatao 9 yametangazwa.

MWISHO.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni